Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya
Ufundi Stadi (VETA) imewahamasisha madereva bodaboda na Bajaji nchini kupata
mafunzo ya udereva kwenye vyuo vya VETA nchini ili kukidhi vigezo vya kupata leseni
za kuendesha vyombo hivyo.
Hamasa hiyo imetolewa Julai 24, 2022 jijini Dodoma wakati wa Kongamano la Kuimarisha Ushiriki wa Waendesha Bodaboda na Bajaji katika Sensa ya Watu na Makazi Agosti 2022 ambapo VETA ilialikwa kufanya maonesho.
Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati, Ndugu John Mwanja, aliiwakilisha VETA kwenye kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Anthony Mtaka.
Kongamano hilo limejumuisha waendesha bodaboda na Bajaji zaidi ya 3000 kutoka Mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara.
No comments:
Post a Comment