CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Monday 31 October 2022

Chuo cha VETA cha Wilaya ya Pangani chakamilika kwa asilimia 95

 

Mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Pangani mkoani Tanga umefikia asilimia 95 ya utekelezaji wake huku mafunzo yakitarajia kuanza kutolewa mwezi Januari, 2023.

Mradi wa Ujenzi wa Chuo hicho unatekelezwa na Chuo cha VETA Dar es Salaam kwa kutumia nguvu kazi ya ndani yaani Force Account.

Mradi huo unakadiriwa kutumia  takribani shilingi bilioni 2.8 hadi kukamilika kwake.

Chuo cha VETA Wilaya ya Pangani kitatoa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana wa wilaya ya Pangani na maeneo ya jirani ambapo vijana watapatiwa ujuzi kupitia fani mbalimbali na hatimaye kuwawezesha kuajiriwa au kujiajiri kwenye shughuli mbalimbali za kiuchumi ili  kujipatia kipato na kuweza kuendesha maisha yao na kukuza uchumi wa Wilaya ya Pangani na taifa kwa ujumla.

Ujenzi wa chuo hicho unajumuisha majengo kumi na saba (17) kama ifuatavyo: Karakana ya ushonaji, Karakana ya Kompyuta na uhazili, Kakarana ya ufundi wa magari na uchomeleaji vyuma, Karakana ya umeme na uashi, Jengo la Utawala( administration block), Madarasa  mawili ( General class room), Bwalo la chakula na jiko, Nyumba ya Mkuu wa Chuo, Bweni la wasichana, Bweni la wavulana, Stoo, Jengo la jenereta, Vyoo vya watumishi, Vyoo vya wanafunzi wavulana, Vyoo vya wanafunzi wasichana na Kibanda cha ulinzi.

MWONEKANO WA MAJENGO KATIKA CHUO CHA UFUNDI STADI CHA WILAYA YA PANGANI

      Jengo la utawala( administration block)

      Kakarana ya ufundi wa magari na uchomeleaji vyuma

      Karakana ya umeme na uashi


      Bwalo la chakula na jiko

      Nyumba ya Mkuu wa chuo

      Bweni la wasichana

      Bweni la wavulana

No comments:

Post a Comment