Mamlaka
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA imesaini makubaliano na kampuni ya
mtandao wa simu wa AitelTanzania kwa lengo la kuimarisha mafunzo ya ufundi
satdi kwa njia za kidigiatali (VSOMO APP), programu ambayo itawawezesha vijana
kujifunza stadi mbalimbali popote walipo kwa kutumia simu za mkononi au
vishikwambi.
Makubaliano
hayo yamesaini leo, tarehe 5 Mei, 2026 na Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony
Kasore na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Charles Kamoto
kwenye ofisi za Airtel Tanzania, Kinondoni jijini Dar es salaam.
Kwa
mujibu wa hati ya makubaliano iliyosainiwa, makubaliano hayo yanalenga kuleta
mabadiliko chanya katika utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi kwa njia za
kidigitali, kwani kupitia VSOMO APP mtu atapata mafunzo ya nadharia (theory)
moja kwa moja kupitia simu yake ya mkononi au kishikwambi, hivyo hatahitaji
kuwa darasani muda wote.
Hati hiyo imefafanua kuwa baada ya kumaliza masomo ya nadharia kwenye
simu, mwanafunzi atachagua chuo chochote cha VETA kilicho ili kukamilisha
mafunzo ya vitendo.Aidha
kupitia VSOMO APP mwanafuzi ataweza kujifunza masomo ya ufundi kwa lugha na Kiswahili au
Kingereza, jambo linalomwezesha mwanafunzi kuelewa kwa urahisi.
Akizungumza
kabla ya kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore
amesema VSOMO APP ni jukwaa kubwa linalowaweza wananchi kupata mafunzo kwa njia
ya kidigitali kupitia teknolojia ya simu,kompyuta na vishikwambi.
“kwa
upande wetu sisi kama VETA tumekuwa tukiutumia mfumo huu,kulingana na jukumu
tulilonalo lakutoa mafunzo mfumo huu
unatusaidia kuwafikia watanzania popote walipo kwa urahisi” amebainisha Kasore.
CPA
Kasore ameongeza kuwa jukwaa la VSOMO APP pia limeunganishwa na mfumo wa Fundi
Connect, unaowawezesha wahitimu wa VETA kusajili ujuzi wao na kuunganishwa moja
kwa moja na wateja, hivyo kuimarisha uhusiano kati ya mafunzo na ajira pamoja
na kusaidia ujasiriamali wa vijana.
Sambamba
na hilo Kasore amesema ushirikiano huo unaunga mkono ajenda ya maendeleo ya
Taifa chini ya Dira ya Maendeleo 2030, na kuimarisha juhudi za Serikali za
kuongeza ajira kwa vijana chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
¬“Tunaishukuru
sana Airtel Tanzania kwa msaada wao endelevu, hasa katika kutoa huduma ya
intaneti na kuwezesha upatikanaji mpana wa VSOMO. Ushirikiano huu umetuwezesha
kuwafikia vijana wengi zaidi kuliko hapo awali. Lakini pia tunaishukuru
Serikali ya kwa kuendelea kuwekeza katika
Elimu na mafunzo ya ya ufundi stadi,” amesema Kasore
Amebainisha
kuwa kupitia VSOMO, VETA imelenga kuwafikia wanafunzi wapya 400 kila mwezi,
kama sehemu ya kuendelea kupanua mafunzo ya ujuzi kidigitali na kuimarisha
ajira kwa vijana nchini.
“Kupitia
VSOMO, tunapanua wigo ili vijana wengi zaidi wapate ujuzi wa vitendo kwa ajili
ya ajira na kujiajiri popote walipo,” amesema
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Charles Kamoto, amesema
ushirikiano huo unaonesha dhamira ya Airtel katika kuendeleza mageuzi jumuishi
ya kidigitali na kupanua upatikanaji wa elimu ujuzi kwa Watanzania.
“Airtel
VSOMO ni jukwaa rasmi la taifa la mafunzo ya ufundi stadi mtandaoni chini ya
VETA. Linawawezesha Watanzania kupata ujuzi wa vitendo wakati wowote na mahali
popote kupitia vifaa vyao vya kidigitali,” amesema Kamoto.
Kamoto
amesisitiza kuwa mchango wa Airtel hauishii kwenye mawasiliano pekee, bali
unajumuisha uwekezaji mpana katika ujumuishaji wa kidigitali, elimu na
uwezeshaji wa vijana.
_“Sisi
Airtel hatujihusishi tu na kutoa huduma ya mtandao. Tunahamasisha kikamilifu
matumizi ya Airtel VSOMO, tunatoa huduma ya bila gharama ya data, na
kuhakikisha gharama si kikwazo kwa Watanzania kujifunza na
kujiendeleza,”_ameongeza
Naye
Beatrice Singano, Mkurugenzi wa mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania
amesema VSOMO inasiadia vijana wengi kujifunza kupitia mtandao huku wakiendelea
na shughuli zao nyinge za uzalishaji.
_“tuliwauliza
vijana wengi wakasema kozi za VETA zina manufaa makubwa kwao, lakini hawana
muda wa kwenda kukaa darasani muda mrefu, hivyo kwa kupitia VSOMO vijana
watatumia muda mchache kusoma kupiti simu zao, huku wakiendelea na shughuli zao
za uzalishaji bila kuathirika”_amesema.
Takwimu
za Airtel zinaonesha kuwa Airtel VSOMO imepakuliwa mara 59,000, ambapo
takribani asilimia 60 ya matumizi yamefanyika kupitia huduma ya bure ya data ya
Airtel. Jumla ya watumiaji 27,194 wamejisajili kwenye jukwaa hilo, huku
wanafunzi 9,539 wakijiunga na programu mbalimbali za ufundi stadi.
Kati
ya hao, wanafunzi 6,723 tayari wamehitimu mafunzo yao, jambo linaloonesha
ongezeko la matumizi na mafanikio katika elimu ya ufundi stadi ya kidigitali.