CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Thursday 25 July 2024

VETA, THT waunganisha nguvu kuandaa vijana katika sekta ya sanaa nchini

 

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo Ya Ufundi Stadi (VETA) na Tanzania House of Talents (THT) zimetia saini hati ya makubaliano, kuanzisha ushirikiano wa kutoa mafunzo katika sekta ya sanaa ili kuwawezesha vijana kuwa na ujuzi unaotambulika rasmi katika sekta hiyo hapa nchini.

Makubalioano hayo yamesainiwa tarehe 25 Julai 2024 na  Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore na Mkurugenzi Mkuu wa THT Kemilembe Mutahaba, katika ukumbi wa mikutano, VETA Makao Makuu, Jijini Dodoma.

Akizungumza kabla ya utiaji saini wa hati hiyo ya ushirikiano, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Kasore amesema sambamba na juhudi ilizoanzisha zikilenga kuboresha sekta ya sanaa nchini, VETA imeona ni vyema kuanzisha ushirikiano na wadau muhimu katika sekta hiyo ili ujengeaji ujuzi kwa vijana uwe wenye matokeo makubwa zaidi.

Amezitaja juhudi zilizofanywa na VETA kwa nia ya kuboresha sekta ya sanaa nchini kuwa ni pamoja na kuandaa mitaala mipya ya ikiwemo ya Utengenezaji wa Filamu (Film Production), Sanaa na Usanifu (Arts and Design), Uandaaji wa Matukio (Events Planning) na Uandaaji Muziki (Music Production).

“THT wako na vijana kwa muda mrefu, wanawafundisha na kukuza vipaji vyao katika sanaa, nasi tumeona ni vyema kushirikiana nao ili kuunganisha nguvu, ili kuwaandaa vijana wa Kitanzania kuwa na ujuzi bora wa sanaa na unaotambulika rasmi,” amesema.

Alisema, uamuzi wa VETA kuandaa mitaala ya sekta ya sanaa na kuanza kutoa mafunzo kwenye sekta hiyo umetokana na taarifa za utafiti wa  soko la ajira kubaini kuwa vijana wengi katika sekta hiyo wamekuwa wakifanya shughuli zao kwa kutumia vipaji walivyonavyo, ubunifu pamoja na ujuzi walioupata katika mfumo usio rasmi.

“Sasa katika kuweka suala hili vizuri tumeona ujuzi huu uweze kutambulika rasmi kwa kuandaa na kuanza kutoa mafunzo yatakayowawezesha vijana kujifunza na kupata vyeti katika eneo hilo,” ameongeza CPA Kasore.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa THT, Kemilembe Mutahaba amesema wameingia makubaliano na VETA waweze kutumia fursa ya mitaala na mafunzo ya VETA ili vijana wanaowaandaa na kukuza vipaji vyao waweze kupata vyeti na kutambulika, kwani wamekuwa wakiwapa mafunzo ya sanaa pasipo kuwapatia vyeti.

“Mara nyingi tumekuwa tukiwapa mafunzo vijana, lakini hatuwapi vyeti vinavyotambulika na Serikali. Tumewekeza bidii zetu kuwawezesha vijana kuajirika kupitia vipaji vyao, kupitia ushirikiano huu tutaweza kuwasaidia kupata vyeti na kutambulika rasmi," amesema.

Naye Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dkt. Abdallah Ngodu alifafanua kuwa mitaala iliyoandaliwa ilizingatia taarifa za utafiti wa soko la ajira uliofanyika mwaka wa fedha 2022/2023 na kubaini kuwa vijana wengi nchini wanafanya kazi za sanaa, hasa muziki bila kupitia kwenye mfumo rasmi wa mafunzo.

Dkt. amesema taarifa za soko la ajira ziliainisha mahitaji ya ujuzi na baada ya kuchakatwa, wataalamu wabobevu kwenye sekta ya sanaa walishirikishwa katika kuandaa mitaala.

Ameongeza kuwa rasimu za mitaalaa zilipelekwa kwenye Kamati ya Ushauri ya Kisekta ili kupitia na kupata maoni na zinatarajiwa kupelekwa kwenye kikao kijacho Bodi kwa idhini, kisha Baraza la Taifa ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kwa ajili ya kuridhiwa na kupewa ithibati.




Friday 5 July 2024

Usikose Kuangalia vipindi vya VETA katika maonesho ya SabaSaba, Saa 11:30 Jioni, TBC na Saa 12:45 Jioni Azam TV.


 

Mafundi nguo wenye ulemavu wapata dili Sabasaba

 

Kuona ni kuamini ndivyo unavyoweza kusema kutokana na umahiri unaooneshwa na vijana wenye ulemavu waliohitimu fani ya ushonaji, ubunifu na teknolojia ya nguo kutoka vyuo vya Veta ambao wamepata fursa ya kuwashonea washiriki na watembeleaji wa Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa maarufu Sabasaba.

Vijana hao Riziki Ndumba na Abdi Kipara wenye ulemavu wa viungo ambao wako katika banda la Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA) mbali ya kueleza namna walivyonufaika na mafunzo pia wameweza kuaminiwa na baadhi ya washiriki na watembeleaji wa maonesho hayo kwa kuwashonea nguo na kujiongezea kipato. Soma zaidi. 

 Chanzo: mtanzania.co.tz


Thursday 4 July 2024

WABUNIFU WAINGIA NA MASHINE ZA KUKAUSHA NA KUTENGANISHA MBEGU MAONYESHO YA SABASABA


 

BRELA yatoa elimu kwa washirki wa VETA Sabasaba kuhusu miliki bunifu

 

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), leo, tarehe 4 Julai 2024, imetoa elimu kwa washiriki wa VETA kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (Sabasaba), kuhusu miliki bunifu.

Akizungumza na washiriki wa VETA kwenye maonesho hayo, Afisa usajili wa BRELA, Stanislaus Kigosi amesema kilichowasukuma kukutana na washiriki wa VETA Sabasaba ni kutokana na kutambua kwamba VETA kuna ubunifu mwingi kutokana na namna ya utoaji mafunzo ya ufundi stadi.

  “Kutokana na VETA kuwa na bunifu zinazo tatua changamoto za kijamii, zinazohusu mambo ya teknolojia na ujasiriamali ndio kilicho tusukuma kuja kutoa elimu hii inayohusu ulinzi wa miliki bunifu," amesema Kigosi.

Naye  Sada Rashidi (Usajili) ameshauri pia kulinda alama za biashara na rajamu (brand) za bidhaa zao.