CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Wednesday 16 November 2022

Vijana 4000 kunufaika na mafunzo ya ufundi stadi kupitia mradi waE4D

 

Jumla ya vijana  4,000 katika mikoa ya Lindi,  Manyara, Dodoma , Dar es salaam  wanatarajia kunufaika  na mafunzo ya ufundi Stadi kwenye fani za Ufundi Bomba wa Viwandani, Uchomeleaji na Mekatroniki kwenye vyuo vya VETA kupitia mradi wa Ajira na Ujuzi kwa Maendeleo ya Afrika(E4D).


                               Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa vya kufundishia iliyofanyika kwenye chuo cha VETA Lindi tarehe 10 Novemba 2022, Mratibu wa mradi wa E4D Ndugu Kabogo Mbuyi amesema mradi huo unalenga kukuza ujuzi na kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini.


 Amesema mradi huo unatekelezwa kupitia Shirika la maendeleo la Ujerumani (GIZ) pamoja na  Ofisi ya Waziri Mkuu,  Kazi, Vijana,  Ajira, na Wenye Ulemavu na unafadhiliwa na GIZ kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU) na Shirika la Misaada na Maendeleo la Korea KOICA kwa gharama ya shilingi bilioni 1.3.


Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa VETA, Ndugu Felix Staki, ambaye alikuwa akimuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA, alisema utekelezaji wa mradi wa E4D utachangia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza udahili, kutoa fursa zaidi kwa vijana kupata ujuzi kupitia mafunzo ya ufundi stadi, kuimarisha ubora wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia vifaa vya kisasa vya kufundishia pamoja na kuongeza ujuzi kwa walimu wa ufundi stadi.


Alisema katika chuo cha VETA Lindi mradi huo unatarajia kunufaisha vijana 700 watakaopata mafunzo ya muda mfupi kwenye fani za Ufundi Bomba pamoja Uchomeleaji na Uungaji vyuma ambapo jumla ya shilingi 228 milioni zimetumika kununulia vifaa.

 


Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bi Zainab Telack, alisema ni matarajio ya Serikali ya Mkoa kuwa vijana watakaohotimu mafunzo hayo watakuwa na ujuzi wa kutosha utakaowawezesha kujiajiri.

 

Naye Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA Lindi, Ndugu  Harry  Mmari, alishukuru GIZ kwa vifaa vilivyotolewa  ambavyo vitasaidia  kutoa mafunzo na kutengeneza ajira kwa vijana .

 

No comments:

Post a Comment