Walimu wa Chuo cha VETA cha Mkoa wa Morogoro (VETA Kihonda)
wametoa mafunzo kwa madereva 47 na makondakta 36 wa kampuni ya Blue Coast kwa
lengo la kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi na weledi ikiwa ni pamoja na
kupunguza ajali zinazotokana na makosa ya kibinadamu.
Mafunzo hayo yametolewa mjini Geita tarehe 19 hadi
24 Desemba, 2022 .
Mwalimu Kiongozi wa Udereva wa Magari Makubwa na
Mabasi wa chuo cha VETA Kihonda, Ndugu William Munuo, amesema madereva na
makondakta hao wamejifunza kwa nadharia na vitendo kuhusu masuala mbalimbali
ikiwemo udereva wa kujihami, huduma kwa wateja na huduma ya kwanza.
Kampuni ya Blue Coast iliyopo mjini Geita inamiliki
magari makubwa yanayohudumia wafanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (Geita Gold
Mine - GGM).
Mafunzo yaliyotolewa ni mwendelezo na jitihada za
Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) katika kuhakikisha kuwa
ujuzi unaotolewa unawafikia wahitaji wote popote walipo.
No comments:
Post a Comment