CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Wednesday 28 December 2022

VETA yatoa mafunzo kwa madereva 47, makondakta 36 wa kampuni ya Blue Coast ya mjini Geita

Walimu wa Chuo cha VETA cha Mkoa wa Morogoro (VETA Kihonda) wametoa mafunzo kwa madereva 47 na makondakta 36 wa kampuni ya Blue Coast kwa lengo la kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi na weledi ikiwa ni pamoja na kupunguza ajali zinazotokana na makosa ya kibinadamu.

Mafunzo hayo yametolewa mjini Geita tarehe 19 hadi 24 Desemba, 2022 .

Mwalimu Kiongozi wa Udereva wa Magari Makubwa na Mabasi wa chuo cha VETA Kihonda, Ndugu William Munuo, amesema madereva na makondakta hao wamejifunza kwa nadharia na vitendo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo udereva wa kujihami, huduma kwa wateja na huduma ya kwanza.

Kampuni ya Blue Coast iliyopo mjini Geita inamiliki magari makubwa yanayohudumia wafanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (Geita Gold Mine - GGM).

Mafunzo yaliyotolewa ni mwendelezo na jitihada za Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) katika kuhakikisha kuwa ujuzi unaotolewa unawafikia wahitaji wote popote walipo.

No comments:

Post a Comment