Rai hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula, tarehe 11.09.2023 alipotembelea chuo cha VETA-Ndolage kwa lengo la kukagua na kujionea ujenzi unaoendelea katika chuo hicho.
Katika ziara hiyo Dkt.Rwezimula alikagua Ujenzi wa jumla ya majengo 6, ambayo ni jengo la karakana ya umeme wa majumbani, bwalo la chakula lenye uwezo wa kuhudumia watu 200 kwa mkupuo, nyumba ya mkuu wa chuo, jiko na mabweni mawili ya wanafunzi wa kike na kiume yenye uwezo wa kubeba jumla ya wanafunzi 160.
Dkt Rwezimula aliongeza kuwa upanuzi wa chuo cha VETA-Ndolage utakaokipandisha hadhi chuo hicho kutoka kuwa VTC na kuwa DVTC ni sehemu pia ya utekelezaji wa mpango Serikali ya awamu ya Sita ya kuhusu utoaji Elimu ya Mafunzo ya Ufundi Stadi ili kuzalisha nguvu kazi yenye Ujuzi utakaowawezesha vijana kujiajiri au kuajiriwa.
Akisoma ripoti ya uendelezaji wa ujenzi, Kaimu Mkuu wa chuo cha VETA-Ndolage, Machumu Kingi Machumu amesema shilingi milioni 903.57 zilitengwa na serikali kwa ajili ya kazi ya upanuzi wa chuo hicho, ambapo mpaka sasa zimetumika shilingi milioni 189.1.
Kumalizika kwa utekelezaji wa upanuzi wa chuo VETA-Ndolage kunatarajiwa kuleta ongezeko la udahili kutoka wanafunzi 70 wa mwaka huu 2023 na kufikia wanafunzi 200 ambapo 160 watapata nafasi ya kukaa bweni na 40 kutwa.
Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, amesema upanuzi huo utahitaji ongezeko la walimu ili kukidhi utoaji Mafunzo, hivyo VETA imejiandaa kuomba vibali vya kuajiri huku akiahidi kutumia walimu wa muda kutoka vyuo vya jirani kusaidia kutoa mafunzo.
Amesema, utekelezaji wa
Upanuzi wa chuo cha VETA-Ndolage
utakwenda sambamba na ongezeko la kozi
za Ufundi Magari, Ufundi Umeme wa Magari, Udereva wa Magari na pikipiki, kozi ya
Uongezaji thamani Mazao ya Chakula ili kuhakikishia wananchi wa Muleba wanapata nguvu kazi yenye ujuzi kwa ajili ya uzalishaji wenye tija.
Chuo cha VETA-Ndolage
kilianza kutoa mafunzo Juni 2020 kwenye fani za Uashi, Uundaji na Uungaji
vyuma, Uhazili na Kompyuta pamoja na Ushonaji, Ubunifu wa Mavazi na Teknolojia
ya Nguo.
No comments:
Post a Comment