CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Thursday 30 November 2023

Maonesho ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya NECTA

 

Wahitimu wa kidato cha nne wahamasishwa kujiunga na kozi za muda mfupi kwenye vyuo vya VETA

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) inashiriki kwenye maonesho ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Baraza la Mitihani la Tanzania(NECTA), yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Novemba hadi 3 Desemba, 2023.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amefungua rasmi maonesho hayo leo tarehe 30 Novemba, 2023, ambapo viongozi mbalimbali wakiwepo Wakuu wa Taasisi zilizoko chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pia wamehudhuria.


Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Dar es Salaam, Ndg. Angelus Ngonyani, amemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA kwenye hafla ya ufunguzi, akiambatana na Mkuu wa Chuo cha VETA Dar es Salaam, Mhandisi Joseph Mwanda.

VETA inatumia maonesho hayo kutoa taarifa mbalimbali za mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa kwenye vyuo vyake na kuhamasisha wananchi, hasa wahitimu wa kidato cha nne mwaka huu, kujiunga na kozi za muda mfupi, katika kipindi cha mpito kabla ya matokeo na/au kuendelea na ngazi zingine za masomo. Mafunzo hayo yatawasaidia  kuwa na hazina ya ujuzi unaowawezesha kuajirika kwa urahisi.

Kupitia maonesho hayo pia VETA inawaelimisha wananchi namna ilivyojipanga katika kuwezesha utoaji wa mafunzo ya amali  kuendana na mabadiliko ya mitaala ya elimu ya Sekondari.


VETA inawakaribisha wananchi wote kutembelea banda lake kwenye maonesho hayo ili kupata taarifa mbalimbali zinazohusu mafunzo ya ufundi stadi na kujionea kwa uhalisia shughuli za mafunzo.





No comments:

Post a Comment