CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Sunday 3 December 2023

VETA yaihakikishia jamii utayari wake utekelezaji wa mabadiliko ya mitaala ya Sekondari

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeihakikishia jamii utayari wake katika utekelezaji wa mitaala mipya ya Sekondari kwa upande wa utoaji mafunzo ya amali.

Meneja Uhusiano wa VETA, Ndg. Sitta Peter, amesema hayo tarehe 3 Desemba, 2023, wakati wa kuhitimisha maonesho ya miaka 50 ya NECTA yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini, Dar es salaam.

Ametaja baadhi ya  majukumu ya VETA kwenye utekelezaji wa mitaala hiyo kuwa ni kuandaa mitaala na vitabu vya kufundishia mafunzo ya amali na kusimamia utoaji wa mafunzo hayo kwa ufanisi.

Amesema, tayari VETA imeshaandaa mitaala, miongozo na vitini kwa ajili ya mafunzo ya amali shule za sekondari, ambayo yanatarajiwa kuanza Januari, 2024.

Sambamba na hilo ametoa wito kwa wahitimu wa darasa la saba na kidato cha nne kujipatia ujuzi katika vyuo vya VETA nchini katika kipindi cha mpito wanachosubiria kuendelea na hatua zingine za masomo.

Amesema ujuzi huo utakuwa akiba kwenye maisha yao na kuwawezesha kujiajiri na kuajiriwa.

 

No comments:

Post a Comment