CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Thursday 29 February 2024

Miti 500 yapandwa katika chuo cha VETA Wilaya ya Uyui

Walimu na wanafunzi katika chuo cha VETA Wilayani Uyui, Mkoani Tabora, tarehe 28 Februari, 2024 wamepanda miti zaidi ya 500 katika chuo cha VETA Wilaya ya Uyui.

Zoezi hilo lililokuwa na lengo la kutunza mazingira na utekelezaji wa maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar limeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Uyui, Mhe. Zakaria Mwansasu ambapo pia Katibu Tawala wa Wilaya ya hiyo Bi Neema Mfugale alihudhuria.

Akizungumza baada ya zoezi la upandaji miti, Mhe. Mwansasu amesisitiza miti hiyo kutunzwa na kuagiza kila mwanafunzi chuoni hapo kukabidhiwa mti kwa ajili ya kuutunza.

“Nakabidhi miti hii naomba kila shimo liwe na mwanafunzi mmoja au wawili ili huo mti ukipotea au kukauka ni lazima urudishiwe. Tusipande miti halafu kesho na keshokutwa miti hiyo inakauka,” amesema.

Ameongeza, “Tunataka tupande miti hii ili kesho na kesho kutwa tukirudi tunasema sisi ndio wanafunzi wa kwanza wa chuo hiki tuliopanda miti hii,”

Naye Kaimu Msajili wa chuo hicho ,ndugu Fedric Phanuel Lukumay amewashukuru Wakala wa Misitu(TFS), Wilaya ya Uyui na Mhifadhi wa wilaya,  kwa kukubali ombi lao la kuwapatia miti hiyo mia tano iliyopandwa chuoni hapo.

Amesema wamepanda miti katika chuo hicho sio tu katika kutunza mazingira, lakini pia katika kuweka mandhari bora na mipaka kuzunguka chuo hicho.








No comments:

Post a Comment