Maadhimisho ya Siku
ya Mazingira Duniani mkoani Tabora yamefanyika leo tarehe 5 Juni 2024 katika
chuo cha VETA Uyui, ambapo zoezi la kupanda miti limefanyika chuoni hapo.
Mkuu wa Wilaya ya Uyui, Mhe. Zacharia Mwansansu ameongoza zoezi hilo la upandaji miti akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambapo jumla ya miti 120 imepandwa chuoni hapo.
Madhimisho hayo yenye
kauli mbiu isemayo "Urejeshwaji wa Ardhi, ustahimilivu wa hali ya Jangwa
na Ukame" yana lengo la kutoa elimu ya utunzaji na uhifadhi wa Mazingira.
No comments:
Post a Comment