CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Monday 10 June 2024

Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 waweka jiwe la msingi Ujenzi wa mabweni chuo cha VETA Namtumbo.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024, Ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava, jana, tarehe 9 Juni, 2024  ameweka  Jiwe la Msingi katika mradi wa ujenzi wa mabweni mawili chuo cha ufundi stadi cha VETA Wilaya ya Namtumbo unaojengwa kwa kutumia nguvukazi ya ndani (force account).

Ujenzi wa mradi huo unaokadiriwa kugharimu shilingi  milioni 800 umefikia asilimia 85.

Jiwe hilo la msingi limewekwa baada ya viongozi wa mbio za  Mwenge kujiridhisha kuwa mradi huo umekidhi viwango vya ujenzi kwa mujibu wa miongozo ya ujenzi wa majengo ya Serikali.

"Mwenge wa Uhuru umefanya ukaguzi wa kina kuhusu nyaraka zinazohusiana na mradi, umetembelea na kujionea miundombinu ujenzi ulipofikia. Tunafanya haya ili kuhakikisha tunabaini ubora na viwango vinavyotakiwa katika mradi husika, thamani ya fedha iliyotumika kama inaakisi maendeleo na uhalisia  wa matokeo ya mradi," amesema Mnzava.

Naye, Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya amesema Mradi wa ujenzi wa mabweni hayo utaongeza idadi ya wanafunzi chuoni hapo kwani  utasaidia katika kutatua changamoto ya wanafunzi wenye nia ya kusoma lakini wanatoka mbali na chuo.

Akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa mradi mabweni hayo, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Privatus Majiyamotoo amesema mradi huo hadi sasa umefikia zaidi ya asilimia 85 katika ujenzi wake ambapo hadi kukamilika unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi mil 800  ambapo chanzo cha fedha hizo ni  Serikali kuu.



No comments:

Post a Comment