Jumla ya wasimamizi wa
vyuo vipya vya VETA wamejengewa uwezo wa uratibu na uendeshaji wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi Stadi ili kuimairisha utoaji mafunzo na kuzalisha wahitimu
mahiri.
Kikao kazi cha kujengeana uwezo kinafanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 18 hadi 19 Juni 2024 katika ukumbi wa Chuo cha VETA Dodoma na kimefunguliwa leo, tarehe 18 Juni, 2024 na Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dkt.Abdallah Ngodu aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA.
Dkt. Ngodu amewahimiza
washiriki hao kufuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizoandaliwa ambazo
zitawawezesha kufanya kazi kwa ufanisi na kuhakikisha malengo ya VETA
yanafikiwa.
“tumekutana hapa kwa ajili ya kukumbushana na kuelekezana misingi tunayopaswa kuifuata na kuiheshimu katika kuhakikisha kazi ya utoaji mafunzo kwa ajili ya kuzalisha Watanzania wenye ujuzi, hasa vijana mnaowahudumia katika vituo vyenu inatekelezwa kwa ufanisi,” amesema.
Afisa Mkuza Mitaala wa VETA, Bi. Happiness Salema, amesema kikao kazi hicho ni sehemu muhimu ya kupeana mrejesho wa utekelezaji wa shughuli za utoaji mafunzo kwenye vyuo vya VETA na kubadilishana uzoefu ili hatimaye kuleta weledi katika utoaji mafunzo.
Mwakilishi wa wasimamizi wa vyuo vinavyoshiriki, ambaye ni Kaimu Msajili wa Chuo cha VETA cha Wilaya ya Ukerewe, Mhandisi Shinzeh Deudedith, ameshukuru uongozi wa VETA kwa kuandaa kikao kazi hicho na kuahidi kuyafanyia kazi mafunzo na maelekezo watakayoyapata.
Kikao kazi hicho
kinahusisha Wasimamizi wa Vyuo vipya 30 ambapo, 26 wanatoka vyuo vya ngazi ya
Wilaya na wanne (4) kutoka vyuo vya ngazi ya Mkoa ambapo mada
zitakazowasilishwa ni pamoja na utekelezaji wa Mitaala, miongozo mbalimbali ya
utoaji wa mafunzo ikiwa ni pamoja na Ufuatiliaji na Tathmini, Mafunzo ya
Uanagenzi kwa Mfumo Rasmi, Uchaguzi wa Wanafunzi, Unasihi na Ushauri wa Mafunzo
na Kazi,Elimu Jumuishi ya Wanafunzi wenye Mahitaji Maalum na Uendeshaji na
Tathmini ya Mitihani.Mada nyingine zitakazowasilishwa ni pamoja na Upangiliaji
Karakana na Utangazaji wa fursa za Mafunzo.
No comments:
Post a Comment