CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Saturday 1 June 2024

Watumishi wa VETA Makao Makuu wapewa mafunzo ya kupambana na majanga ya moto

Watumishi wa VETA Makao Makuu wamepewa mafunzo ya kupambana na majanga ya moto ikiwa ni sehemu ya juhudi za Mamlaka kuhakikisha usalama mahala pa kazi.

Mafunzo hayo yametolewa  tarehe  31 Mei, 2024 katika eneo la VETA Makao Makuu, jijini Dodoma na kuwasirikisha watumishi wa idara na vitengo vyote vya VETA.

Akitoa mafunzo hayo ya kupambana na majanga ya moto, Insp. Stephen Katte kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, mkoani Dodoma amesema majanga ya moto yanaepukika kama wananchi wataweka mkazo katika utayari, umakini na uelewa wa kinga na matumizi ya vifaa vya kuzimia moto.

Hata hivyo Insp. Katte amewataka wananchi kuwa na utamaduni wa kupeleka ramani za majengo yao kwa jeshi lazima moto ili zifanyiwe ukaguzi kabla ya kuanza ujenzi.

“kwasasa tumejikita katika kuzuia majanga ya moto ndio maana tunashauri utuletee ramani ya nyumba kabla ya  kuanza ujenzi ili tuweze kuipitia na kuona kama ina mifumo  ya kung’amua dalili za moto au moshi,” amesema  Insp. Katte.

Kwa upande wake FC Jegu Donias  nae kutoka Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoani Dodoma ameshauri wananchi kuacha kutumia "cable" moja kwa matumizi ya vifaa vinavyotumia umeme kama vile jokofu, feni, runinga, kuchaji simu kwa wakati mmoja.

Ameongeza kuwa  ili kujikinga na majanga ya moto ni vimema maeneo  ya ofisini, nyumbani  na kwenye mikusanyiko ya watu wengi kama sokoni kufungwe vifaa vya kukabiliana na moto.

Sambamba na hilo FC Donias ameelezea mambo ya kufanya Unapogundua moto.

Amesema jambo la kwanza unatakiwa kupiga king’ora, kengele au mayowe ili kuashiria kwamba kuna tukio lisilo la kawaida na kuita Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kupitia namba ya dharula 114.

Furaha Paul ambaye ni Kaimu Meneja Miliki VETA ameshukuru Jeshi la Zimamoto na ukoaji kwa kutuoa mafunzo hayo kwa watumishi wa VETA Makao Makuu na kuwapongeza watumishi wa VETA kwa kushiriki  mafunzo hayo.

No comments:

Post a Comment