Wakala wa Usajili wa
Biashara na Leseni (BRELA), leo, tarehe 4 Julai 2024, imetoa elimu kwa
washiriki wa VETA kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam
(Sabasaba), kuhusu miliki bunifu.
Akizungumza na
washiriki wa VETA kwenye maonesho hayo, Afisa usajili wa BRELA, Stanislaus
Kigosi amesema kilichowasukuma kukutana na washiriki wa VETA Sabasaba ni
kutokana na kutambua kwamba VETA kuna ubunifu mwingi kutokana na namna ya
utoaji mafunzo ya ufundi stadi.
“Kutokana na VETA kuwa na bunifu zinazo tatua changamoto za kijamii, zinazohusu mambo ya teknolojia na ujasiriamali ndio kilicho tusukuma kuja kutoa elimu hii inayohusu ulinzi wa miliki bunifu," amesema Kigosi.
Naye Sada Rashidi (Usajili) ameshauri pia kulinda
alama za biashara na rajamu (brand) za bidhaa zao.
No comments:
Post a Comment