Kuona ni kuamini ndivyo
unavyoweza kusema kutokana na umahiri unaooneshwa na vijana wenye ulemavu
waliohitimu fani ya ushonaji, ubunifu na teknolojia ya nguo kutoka vyuo vya
Veta ambao wamepata fursa ya kuwashonea washiriki na watembeleaji wa Maonesho
ya 48 ya Biashara ya Kimataifa maarufu Sabasaba.
Vijana
hao Riziki Ndumba na Abdi Kipara wenye ulemavu wa viungo ambao wako katika
banda la Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA) mbali ya kueleza namna walivyonufaika
na mafunzo pia wameweza kuaminiwa na baadhi ya washiriki na watembeleaji wa
maonesho hayo kwa kuwashonea nguo na kujiongezea kipato. Soma zaidi.
No comments:
Post a Comment