CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Tuesday, 7 January 2025

VETA, VTA washirikiana kutoa mapendekezo ya uboreshaji Sheria ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Amali Zanzibar

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi (VETA) pamoja na Mamlaka ya Elimu ya Mafunzo ya Amali Zanzibar (VTA), jana, tarehe 6 Januari 2025, wamekutana katika ukumbi wa mikutano VETA Makao Makuu, jijini Dodoma kwa dhumuni la kujadiliana juu  mambo ya kupendekeza katika maboresho ya sheria   ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Amali Zanzibar.

Mkurugenzi wa VTA, Dtk Bakari Silima amesema uboreshaji huo wa sheria unahusiana na uundwaji wa Mamlaka ya Uthibiti wa vyuo vya Amali vya serikali na binafsi na sheria nyingine itakuwa ya kuunda Taasisi ya kuendeleza vyuo vya amali vya serikali. 

“Hivi sasa tupo katika hatua ya kuandaa rasimu mbili za kisheria ili kutenganisha baina ya jukumu la usimamizi na udhibiti ubora wa mafunzo ya amali na jukumu la utoaji wa mafunzo kama ilivyo hivi sasa hapa Tanzania Bara, hivyo tumeona ni jambo muhimu kushirikiana nanyi (VETA);katika kuboresha sheria hizo kwani tuna amini nyinyi mnauzoefu wa muda mrefu" amsema Dkt Silima.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi wa VETA Dkt Abdallah Ngodu akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA, amepongeza VTA kwa hatua madhubuti walizo chukua na kuamua kuishirikisha Menejimenti ya VETA katika mchakato huo wa uboreshaji sheria ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Amali Zanzibar.

Aidha Dkt Ngodu ameleza  majukumu ya VETA kisheria kwasasa yamebaki manne.

“Ifahamike kwamba majuku ya VETA kisheria ni haya kuratibu,kukuza  Elimu na mafunzo ya ufundi stadi, kusimamia mfuko wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na uandaaji mitaala" amesema Dkt Ngodu.

Mamlaka ya Elimu  ya Ufundi na Mafunzo ya Amali ilianzishwa chini ya Sheria ya Mafunzo ya Amali mwaka 2005 ikiwa na majuku ya kupanga,kusimamia,kudhibiti(kurekebu),kuratibu, kuendeleza na kutoa Mafunzo ya Amali Zanzibar.



No comments:

Post a Comment