CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Friday 7 May 2021

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA FAINALI ZA MASHINDANO YA KITAIFA YA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UBUNIFU (MAKISATU) 2021

 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akiwa ameambatana na viongozi wengine wa Serikali alipotembelea mabanda Wabunifu wa Vyuo vya Ufundi Stadi na Mfumo usio Rasmi kwenye finali za Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU), leo tarehe 7 Mei 2021.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akipata maelezo kutoka kwa Mwalimu Emmanuel Bukuku wa Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma Dar es Salaam kuhusu Ubunifu wa Maabara ya Fizikia inayohamishika kwenye fainali Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ( MAKISATU). Mwalimu Bukuku anashiriki fainali za MAKISATU katika kundi la Vyuo vya Ufundi Stadi akiwa na Ubunifu wa Maabara hiyo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akijaribisha begi la shule lililotengenezwa kwa   kutumia mabaki ya mifuko ya saruji. Mabegi hayo ambayo pia yana Mfumo wa kuchaji tochi na simu kwa kutumia nguvu ya jua (Solar) yamebuniwa na kikundi cha Soma Factory cha Mwanza. Soma Factory wanashiriki fainali za MAKISATU katika kundi la Mfumo usio Rasmi.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu akimpongeza Dkt. Abdallah Nyangalio, Mbunifu asiyeona aliyebuni Kifaa cha Kutungia Uzi na kufanikiwa kuingia fainali za MAKISATU kwa Ubunifu huo.

Ziara ya Wajumbe wa Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwenye Fainali za MAKISATU leo, tarehe 7 Mei 2021.  Kulia ni Mwalimu Fredrick Uliki wa Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma Kihonda, akitoa maelezo kuhusu Ubunifu wa mashine ya kusaga karanga.


Ernest Maranya kutoka Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma Dar es Salaam akiwaelezea Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Ubunifu wa dawa ya fangasi. Wajumbe hao wametembelea Maonesho ya Ubunifu katika fainali za MAKISATU, leo tarehe 7 Mei 2021.


Patrick Kitosi kutoka Iringa, Mbunifu wa Mfumo usio Rasmi akitoa maelezo kwa Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu ubunifu wake wa Mashine ya Kukusanya Sumu ya Nyuki. Wajumbe hao walitembelea Fainali za Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) leo, tarehe 7 Mei 2021


Waziri wa Elimu akiwa katika Picha ya pamoja na wabunifu


No comments:

Post a Comment