CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Friday 1 October 2021

Kutana na Yuda Basil Temba mhitimu wa VETA anayebuni sakiti mbalimbali za kusaidia viwanda

 


Yuda Basil Temba alizaliwa mnamo mwaka 1980 na kujiunga na Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma Moshi (VETA Moshi) katika fani ya Ufundi wa Umeme wa Majumbani (Electrical Installation) na  baadaye Chuo cha Ufundi Stadi Arusha (VETA Arusha-Oljoro) katika fani ya Ufundi wa Umeme wa Magari (Auto electrical).

Baada ya kumaliza chuo alifanikiwa kufanya kazi katika viwanda na migodi ikiwemo Buzwagi na Geita Gold Mining.

Kutokana na ujuzi na uzoefu alioupata chuoni na katika viwanda na migodi hiyo, Temba alipata  mawazo ya kubuni vitu mbalimbali vya kusaidia utendaji kazi katika viwanda mfano mashine za kusaga mawe (crusher) na za kuchenjua dhahabu.

Temba anasema kupitia ubunifu huo, aliweza kujikwamua na tatizo la ajira ambapo alifanikiwa kufungua duka la vifaa vya umeme na kubuni saketi mbalimbali za viwandani mkoani Geita. Baadaye, alifanikiwa kufungua karakana ndogo mkoani Geita na kuajiri  vijana  tisa, watatu kati yao wakiwa ni wahitimu wa VETA.

Baada ya karakana hiyo kufanya vizuri, alifanikiwa kufungua kampuni inayojishughulisha na utengezaji wa mashine za Elution za kuchenjulia dhahabu kwa wachimbaji wadogo na wa kati,  mashine ambazo aliweza kuzifunga  ndani na  nje  ya nchi kama vile DR Congo na Mauritania.

Temba anaishukuru  VETA  kwani  licha ya kumuwezesha kupata ujuzi na umahiri katika ufundi stadi pia  alifanikiwa  kuingia kwenye Mashindano  ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu( MAKISATU 2020) ambapo alifanikiwa kuwa  mshindi wa  tatu katika kundi la Wabunifu wa Vyuo vya Ufundi stadi.

Anawashauri vijana wote na wahitimu wote wa vyuo mbalimbali kujifunza ufundi stadi ili kuwakwamua katika tatizo la ajira. Pia anaiomba serikali kuwawezesha wabunifu ili kuleta mabadiliko ya haraka kwenye sekta ya viwanda.


No comments:

Post a Comment