CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Tuesday 12 December 2023

MKATABA WA KUUNDA MABARAZA YA WAFANYAKAZI WA VETA WAHUISHWA

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) na Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu,Sayansi, Teknolojia, Habari, Ufundi Stadi na Utafiti (RAAWU)wametia saini Mkataba wa Kuunda Mabaraza ya Wafanyakazi wa VETA.

Hafla ya utiaji saini imefanyika leo tarehe 12 Desemba, 2023, katika Ofisi za VETA Makao Makuu jijini Dodoma na kushuhudiwa na viongozi wa VETA na RAAWU.

Kusainiwa kwa Mkataba huo wa miaka mitatu (2023 – 2026) kunatoa fursa ya kuanza kwa mchakato wa kuunda mabaraza ya Wafanyakazi wa VETA kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu za ushirikishwaji wa Wafanyakazi mahala pa kazi.

Katibu wa RAAWU Taifa, Ndg. Joseph Sayo, amesema RAAWU itaendelea kushirikiana na uongozi wa VETA katika kuhakikisha malengo ya VETA yanafikiwa na masuala yanayohusu wafanyakazi yanashughulikiwa kwa wakati.


Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Prosper Mgaya, amesema VETA itatimiza wajibu wake katika kutekeleza Mkataba huo na kuushukuru uongozi wa RAAWU kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa VETA.

Mkataba wa Kuunda Mabaraza ya Wafanyakazi ulioisha muda wake ulidumu kwa miaka mitatu (2020 – 2023).

No comments:

Post a Comment