CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Sunday 10 March 2024

MBUNGE AAHIDI MKOPO WA PIKIPIKI 200, BAJAJI 10 KWA WAHITIMU WA UDEREVA VETA MARA

Mbunge wa Musoma Mjini, Mhe. Vadastus Mathayo, ameahidi kuwawezesha mkopo wa pikipiki 200 na bajaji 10 wahitimu wa udereva wa chuo cha VETA Mara.

Mhe. Mathayo ametoa ahadi hiyo wakati wa mahafali ya wahitimu 220 wa udereva wa bodaboda na bajaji yaliyofanyika tarehe 9 Machi,2024 katika chuo Cha VETA Mara ambapo Mbunge huyo alikuwa Mgeni Rasmi.

Mahafali hayo yalihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe.Dkt. Khalfan Haule, Mstahiki Meya wa Musoma Mjini Mhe. William Gumbo na viongozi wengine Wilayani hapo ambao wamempongeza Mbunge huyo kwa kufadhili mafunzo kwa madereva hao.

Mkuu wa Wilaya Mhe. Dkt. Khalfan Haule amewahimiza madereva hao kuzingatia yote waliyojifunza na kuagiza chuo hicho kuanzisha kozi ya ukarimu kwa ajili ya kuhudumia mbuga ya Taifa Serengeti.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha VETA Mara, Martin Mollel amesema chuo chake kitaimarisha utoaji mafunzo kwenye sekta ya utalii na ukarimu. 

Amesema chuo hicho kimeanzisha kozi za muda mfupi za Uandaaji Chakula, Mauzo na Huduma ya Chakula na Vinywaji, Uhazili pamoja na TEHAMA ambapo amewakaribisha wananchi kujipatia mafunzo katika Chuo cha VETA Mara.

No comments:

Post a Comment