Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa chuo cha VETA
Namtumbo, wakati wa hafla ya kukabidhi misaada hiyo, tarehe 28 Machi 2024,
Mwalimu wa fani ya Uashi kutoka chuo hicho, Salim Dendea, amesema wamefanya
hivyo kwa kutambua umuhimu wa kufanya
jambo ili kuwawezesha wanafunzi hao kupata elimu katika mazingira rafiki.
Aidha Dendea amewataka wadau na taasisi nyingine
za serikali na binafsi, kuiunga mkono shule hiyo, ili kuwasaidia wanafunzi hao hasa
wenye mahitaji maalum kila mara wanapoona inawezekana.
Akisoma risala kwa niaba ya uongozi, walimu na
wanafunzi wa Shule ya Msingi na Ufundi Namtumbo, Mwalimu Bibiana Adam Boyanza,
Msimamizi na Mkuu wa Kitengo cha Watoto wenye Mahitaji Maalum amewataka wadau
wengine kuendelea kuwaunga mkono, huku akikishukuru chuo cha VETA Namtumbo kwa
msaada walioutoa na kuwataka kuendelea kuwasaidia kwa kuwa bado wana mahitaji
mengine kama upungufu wa madawati,viwanja vya michezo na visima vya maji ya
uhakika.
“ni rai yangu kuwaita wadau mbalimbali kama
walivyofanya VETA kuja kutuunga mkono, na kwa kuwa VETA mnahusika na kutoa
mafunzo ya ufundi mnaweza kutusaidia zaidi, na kama mnavyoona kitendo hiki
kimeonesha kwamba walemavu sio kwamba hawawezi bali wanaweza wakiwezeshwa,”
amesema.
Naye Noel Hassan Kinonono, mwanafunzi wa darasa la
sita shuleni hapo ameishukuru VETA Namtumbo kwa kuwapa sare hizo na kutoa wito
kwa Serikali kuwasaidia kutatua kero mbalimbali zinazowakabili ikiwepo ya
upungufu wa walimu wa Ufundi katika shule yao.
No comments:
Post a Comment