MAADHIMISHO YA KITAIFA YA ELIMU, UJUZI NA UBUNIFU
Prof. Mkenda
alipotembelea banda la VETA
Waziri wa Elimu,
Sayansi na Teknolojia, Mhe.Prof. Adolf Mkenda, akipata maelezo kutoka kwa
Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA. Anthony Kasore juu ya utoaji wa mafunzo ya ufundi
stadi pamoja na ubunifu alipotembelea banda la VETA kwenye Maadhimisho ya
Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu tarehe 27 Mei, 2024.
Mhe. Mkenda
amepongeza utoaji wa mafunzo kuendana na mahitaji ya soko la ajira na kuonesha
kuvutiwa na mafunzo ya Mekatroniki yanayotolewa katika Chuo cha VETA Kipawa
pamoja na mafunzo kwa wafanyakazi wa majumbani yaliyoanza kutolewa katika vyuo
vya VETA Tanga na Dodoma.
Akiwa kwenye banda la
VETA, Mhe. Mkenda amempongeza Mwalimu wa Chuo cha VETA Kigoma Innocent Maziku
kwa kubuni kifaa cha kusaidia kuongeza usikivu kwa watu wenye usikivu hafifu na
kutoa wito kwa Taasisi na wadau wanaohusika na uendelezaji ubunifu nchini
kuwezesha ubunifu huo kufikia wahitaji ikiwemo wanafunzi wenye changamoto hiyo.
VETA inashiriki kwenye Maadhimisho ya Kitaifa
ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu jijini Tanga ambapo Mhe. Mkenda amefungua rasmi
maadhimisho hayo yaliyoanza tarehe 25 Mei 2024 na yanatarajiwa kuhitimishwa
tarehe 31 Mei, 2024.
No comments:
Post a Comment