Mamlaka ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeshauriwa kuongeza nguvu zaidi katika kutoa
mafunzo ya wataalamu wa huduma za hotel, kwani uhitaji bado ni mkubwa hapa
nchini.
Ushaur huo umetolewa, tarehe 24 Mei,2024 na Naibu Waziri wa Madini,
mheshimwa Dkt Steven Lemomo Kiruswa,
alipotembelea banda la VETA, katika viwanja vya AICC, Jijini Arusha ambapo Jukwaa la Tatu la Kuwezesha
Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini likiendelea.
"Nashauri VETA
muongeze nguvu zaidi katika kutoa mafunzo kwa wahudumu wa hoteli, hasa eneo la
ukarimu ili kupata vijana wengi wenye weledi na sifa za kuajirika katika hoteli
hapa nchini" amesema Dkt Kiruswa.
Ushauri huo umekuja
baada ya mwalimu Hainem Muro kutoa maelezo kwa Naibu Waziri juu ya mafunzo ya
fani ya Utalii na Huduma za za Hoteli nayotolewa na chuo cha VETA cha Hoteli na
Utalii (VHTTI), kilichopo Njiro, Jijini Arusha.
No comments:
Post a Comment