CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Thursday 20 June 2024

VETA Iringa ladies yaahidi ushindi

 

VETA Iringa ladies, leo tarehe 20 Juni 2024, imenza michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa wa Timu za Wanawake za Mpira wa Miguu katika hatua za makundi katika dimba la Jamhuri Jijini Dodoma, huku ikiahidi kutwaa ushindi.

Timu hiyo ambayo imeapa kutwaa kombe na kuiheshimisha VETA, leo imecheza na timu ya Tutes Academy ya mkoani Songea, ambapo kwa taabu sana imekubali kupoteza mchezo huo kwa kufungwa bao 1 kwa 0.

Akizumnguza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, kocha wa timu hiyo, mwalimu Laison Tuyembe, amesema licha ya kupoteza katika mchezo wao wa kwanza wa leo, wanatazamia kufanya vizuri zaidi katika michezo itakayofuata.

“leo tumepoteza kwa kukubali kufungwa goli 1 kwa 0 na wenzetu kutoka mkoani Songea, lakini tuna imani kubwa tutafanya vizuri katika mechi zilizobaki na kutinga hatua ya nusu fainali na hatimae fainali na kutwaa ubingwa wa ligi hii” amesema kocha Laison

Kwa upande wake kapteni wa timu hiyo, Jaqueline Laizer amesema anaimani watafanya vizuri katika michuano hii kama walivyofanya huko Iringa na kuweza kuibuka Kidedea na kuwakilisha mkoa wa Iringa katika ligi hii ya mabingwa wa mikoa wanawake ambayo imeanza kutimua vumbi Jijini Dodoma.

“Ni kweli leo tumepoteza katika mchezo wetu ila tunaamini tutafanya vizuri zaidi katika hatua zinazofuata,” amesema.

 Mkurugenzi wa timu ya VETA Iringa ladies, Ramadhani Mahano ameshukuru uongozi wa chuo cha VETA Iringa kwa kufanikisha timu hiyo kushiriki kikamilifu katika michuano hiyo tangu mkoani Iringa na hatimaye kushinda na kuwa wawakilishi wa Mkoa wa Iringa katika ligi hiyo ya mbingwa wa mikoa wanawake.


Ligi hiyo inadhaminiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Fountain Gate Academy ya Jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment