Mhitimu wa fani ya mavazi na ubunifu wa nguo kutoka chuocha VETA Songea Riziki Ndumba akichukua vipimo vya nguo kwaajili ya kumshonea nguo Esther Peter Mgale mkazi wa ubungo Jijini Dar es salaam baada ya kutembelea banda la VETA katika viwanja vya J.K. Nyerere tarehe 29 Juni 2024.
Esther Mgale amejikuta
akipigwa na butwaa baada ya kuona Riziki
mwenye ulemavu wa viungo ana uwezo mkubwa wa kushona nguo bila kuhitaji msaada
wa mtu mwingine kuanzia hatua za upimaji wa vipimo vya nguo, kukata nguo kwa
kutumia mkasi, kutunga uzi kwenye sindano na hatimaye kushona nguo iliyokamilika.
“kwa kweli nimepatwa na mshangao kumuona
kijana Riziki akiweza kushona nguo bila kuhitaji msaada wa mtu mwingine , kweli
hii nimara yangu ya kwanza kuja kwenye maonesho haya, nawasihii wakazi wenzangu
wa Dar es salaam wafike katika banda la VETA kuna vitu vizuri” amesema Esther
VETA wapo katika maonesho hayo tangu tarehe 28 Juni mpaka yatakapo fikia kilele chake tarehe 13 Julai 2024.
No comments:
Post a Comment