CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Sunday, 23 February 2025

VETA YATANGAZA MAADHIMISHO YA MIAKA 30

 

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, akizungumza na waandishi wa Habari leo Februari 21,2025 katika Chuo Cha VETA Mkoani Singida kuelekea maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanziahwa Kwake mwaka 1995.

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetangaza rasmi maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1995.

Akizungumza na wanahabari leo, tarehe 21 Februari 2025, katika Chuo cha VETA Singida, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, amesema maadhimisho hayo yataangazia mafanikio, changamoto, na mustakabali wa elimu ya ufundi stadi nchini.

CPA Kasore amesema kuwa katika kipindi hiki vyuo vya VETA vilivyoenea kwenye mikoa na wilaya nchini kote vitatoa huduma ya ufundi bure ya ukarabati wa miundombinu ya Serikali kama majengo ya hospitali, zahanati, shule, ofisi za umma pamoja na kwa watu wasiojiweza ikiwa ni sehemu ya maadhimisho na kuonesha mchango wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwenye jami.

Bonyeza hapa kusoma zaidi.


No comments:

Post a Comment