Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)
chini ya ufadhili wa ofisi ya Waziri
Mkuu – Kazi ,Vijana, Ajira Wenye Ulemavu imezindua awamu ya tatu ya zoezi la kurasimisha ujuzi wa mafundi
wasiopungua 3,900 nchini.
Akizungumza
wakati wa uzunduzi wa zoezi hilo katika mikoa ya Morogoro, Dar es salaam, Pwani, Lindi na
Mtwara, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri
Mkuu Kazi ,Vijana, Ajira na
Wenye Ulemavu Mh. Anthony Mavunde kutumia vyema fursa hiyo kwani itawawezesha
kuboresha kazi zao na kuzifanya zikubalike kwenye mfumo rasmi.
Alisema kupitia
zoezi hilo mafundi waliopata ujuzi kupitia mfumo usio rasmi watafanyiwa
tathmini kulingana na ujuzi walionao
kisha kupewa mafunzo kuziba mapungufu na hatimayekutunukiwa vyeti ambavyo
vitawawezesha kutambulika na kukubalika katika mfumo rasmi wa ajira.
Mh
Mavunde aliongeza kuwa asilimia zaidi ya 68% ya watu hapa nchini ni vijana na
ndio maana serikali imeamua kuandaa mpango huo na kuwekeza kwao hasa katika
kuelekea katika uchumi wa viwanda kwani wao ndiyo nguvu kazi inayotegemewa.
Alisema
miongoni mwa faida za programu hii ni kuwasaidia
mafundi waliojifunza kupitia sehemu za kazi (wanagenzi) kupata kazi zenye staha
na kuwajengea wanagenzi sio tu uwezo wa kushiriki na kushindana kikamilifu
katika soko la ajira, lakini pia kuinua tija mahali pa kazi na kusaidia
waajiri/wenye makampuni kukidhi viwango katika eneo la rasilimali watu.
Mkurugenzi wa
Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA Bi.
Leah Dotto aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA wakati wa hafla hiyo ya ufunguzi, alisema awamu ya tatu ya zoezi hili litahusisha mikoa
mitano ambayo ni Morogoro, Dar es salaam,
Pwani, Lindi na Mtwara.
Alisema jumla ya
wanagenzi 22,367 walijitokeza kufanyiwa tathimini ya ujuzi wao ambapo wanawake walikuwa
2,320 (sawa na 10.4%) na wanaume 20,047 (sawa na 89.6).
Kwa mujibu wa
Mkurugenzi huyo, kati ya wanagenzi walioomba kufanyiwa tathmini ya ujuzi wao,
jumla ya wanagenzi 14,424 (sawa na
64.5%) walikidhi vigezo vya kufanyiwa tathmini lakini kutokana na bajeti
iliyopo, zoezi hilo litahusisha kuwafanyia tathmini wanagenzi 3,900 tu kati ya
waliokidhi vigezo.
Aliiomba
serikali kuwezesha zoezi hilo kuwafikia wanagenzi wengine wenye sifa waliowekwa
kwenye orodha ya ziada (Reserve list).
Alisema VETA inatarajia
kuongeza wigo wa mafundi wanaofanyiwa tathmini ya ujuzi ili kuwafikia mafundi
katika nyanja nyingine kama Ushonaji, Ufundi bomba, Uungaji na Uundaji vyuma
(Welding and Metal fabrication), urekebishaji wa bodi za magari (Auto body
repair) na fani nyingine ambazo hazikuweza kufikiwa katika zoezi la awamu hii.
Naye Mbunge wa
Jimbo la Mtwara Vijijini Mh. Hawa Ghasia alisema ana uhakika kuwa baada ya
mafunzo hayo ,vijana hao watakuwa chachu ya kukuza uchumi na hasa kukukuza
fursa za ajira kwa vijana wa mkoa wa Mtwara.
No comments:
Post a Comment