CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Tuesday 14 November 2023

KOICA YATEMBELEA VETA KUJIFUNZA SHUGHULI ZA UTOAJI MAFUNZO YA UFUNDI STADI


 Ujumbe kutoka Korea ya Kusini ukiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Korea (KOICA) Tanzania, Bi. Jieun Seory umetembelea VETA ikiwa ni mwendelezo wa ziara yao ya kujifunza shughuli za utoaji mafunzo ya ufundi na ufundi stadi nchini.

Kupitia ziara hiyo leo tarehe 14 Novemba, 2023, Ujumbe huo umetembelea Ofisi za VETA Makao Makuu na kupata taarifa ya Mamlaka pamoja na kutembelea chuo cha VETA Dodoma kujionea namna mafunzo yanavyotolewa pamoja na miundombinu inayotumika chuoni hapo.

Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Noel Mbonde amesema Serikali ya Korea Kusini ina mpango wa kujenga chuo cha ufundi mkoani Morogoro chenye hadhi ya Kimataifa kitakachotoa ujuzi kupitia programu mbalimbali za kipaumbele katika kukuza uchumi.

 “Ujumbe huu umekuja mahsusi kujionea hali halisi ya utoaji wa mafunzo kwenye vyuo vya ufundi hapa nchini na kupata maoni yetu juu ya kile tunachohitaji kiwepo kwenye chuo wanachotarajia kukijenga,”amesema

Dkt. Mbonde amesema ujumbe huo wa KOICA utaendelea na ziara kwenye vyuo mbalimbali vya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi pamoja na vyuo vya Maendeleo ya wananchi na hatimaye kujadiliana na Wizara ya Elimu na kukubaliana juu ya ujenzi wa chuo hicho.



No comments:

Post a Comment