Wito umetolewa kwa
makampuni na wadau wa sekta ya madini kujitokeza kufadhili mafunzo ya ufundi
stadi yanayotolewa na VETA chini ya programu maalum ya Mafunzo Jumuishi kwa
ajili ya Sekta ya Madini (IMTT).
Wito huo umetolewa na
Rais wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kiliomo Tanzania (TCCIA), Vicent Bruno
Minja, wakati wa mdahalo wa siku ya kwanza ya Jukwaa la Tatu la Ushirikishwaji
wa Tanzania katika Sekta ya Madini, linalofanyika ukumbi wa AICC, Jijini
Arusha, tarehe 22 hadi 24 Mei, 2024.
Kwa kutambua umuhimu wa
mafunzo hayo, Minja ameishauri Serikali na wadau wa madini kuona ni namna gani
mafunzo hayo yanaweza kuendelezwa na kuenezwa katika vyuo vingine badala ya
kuishia kwenye chuo cha VETA Moshi pekee, ambacho sasa kinatekeleza mpango huo
wa mafunzo.
“Nashauri Mwanza na
Mbeya na wao wawezeshwe kutoa kozi zinazohusiana na masuala ya madini kuliko
kuiachia Moshi peke yake,” amesema.
Akifungua Kongamano hilo, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde ametoa rai kwa Watanzania kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya madini.
Maonesho hayo
yanakwenda sambamba na maonesho ya shughuli na huduma mbalimbali zinazohusiana
na sekta ya madini ambapo VETA inashiriki kwenye kongamano pamoja na maonesho.
Mkurugenzi wa VETA
Kanda ya Kaskazini, Monica Mbele, amemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA kwenye
hafla ya ya ufunguzi.
VETA inatumia maonesho
hayo kutoa taarifa mbalimbali za mafunzo ya Ufundi Stadi, hususani yale
yanayolenga kuandaa nguvukazi yenye ujuzi kwa ajili ya Sekta ya madini kama
yanavyotolewa katika vyuo vyake vya Moshi na Shinyanga.
No comments:
Post a Comment