MAMLAKA ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi(VETA)
ikishirikiana na wadau kutoka viwandani vya umeme na umeme wa magari wametoa
maendeleo ya mradi huo kwa wadau wa viwanda.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa kanda ya Dar es
Saalam, ndugu Habibu Bukko wakati akizungumza na wadau wa viwanda vya umeme na umeme
wa magari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa mafunzo hayo yanaumhimu mkuwa
kwa viwanda kwani mafunzo hutolewa kwa umahili mkubwa kwa walichaguliwa
kujifunza mafunzo hayo kutokana na mahitaji ya kiwanda.
Bukko amesema kuwa mafunzo yanayotolewa ni ya
vitendo zaidi (Hands & Skills) chini ya Mradi wa ushirikiano baina ya VETA
na Kampuni ya Handwerkammer Humbarg ya Ujeruman.
Amesema kuwa utaratibu wa mafunzo hayo yamaendaliwa
kutoka na vyuo vya mafunzo ya ufundi Stadi.
Mkurugenzi wa kanda ya Dar es Saalam, Habibu Bukko
akizungumza katika mkusanyiko wa wafanyakazi,viongozi wa VETA pamoja na
(Wanagenzi) wanafunzi wanafanya mafunzo yao katika viwanda mbalimbali hapa
nchini waliojiunga katika mradi wa wanagnizi(APPREUTICESHIP) jijini Dar es
Salaam leo. Amesema kuwa mradi huo unawajulisha wanafunzi wanataka kujiunga na
mafunzo hayo katika chuo cha Veta na kufanya kazi katika viwanda mbalimbali
hapa nchini kuwa mafunzo hayo hayana gharama yoyote na unajifunza katika
kiwanda unachohitaji kutokana na taaluma yako.
Baazi ya wadau kutoka viwandani wakimsikiliza Mkurugenzi wa
kanda ya Dar es Saalam, Habibu Bukko jijini Dar es Salaam leo.
Meneja wa Mradi wa Appreaticeship kutoka kampuni ya
Handwerkammer Humbarg ya Ujeruman, Maltin Mac Mahon akizungumza na wadau wa
Veta jijini Dar es Salaam leo na akielezea jinsi alivyowafundisha wanafunzi wa
veta ambao wapo na ambao hawapo viwandani hapa nchini kutengeneza vitu vya
umeme pamoja na umeme wa magari hapa nchini pamoja na vitu mbalimbali vilivyopo
katika viwanda mbalimbali kutokana na mahitaji ya kiwanda husika.
Wadau wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mradi wa
Appreaticeship kutoka kampuni ya Handwerkammer Humbarg ya Ujeruman, Maltin Mac
Mahon (Mbele) jijini Dar es Salaam leo wakati wa kuwapa maendeleo ya mradi wa
wanagenzi.(Appreaticeship).
Baadhi ya wadau wakisikiliza maada katika mkutano
wa kuwapa maendeleo ya mradi wa wanagenzi (Appreaceship) jijini Dar es Salaam
leo.
Wanafunzi wanafanya mafunzo katika viwanda
mbalimbali hapa nchini wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa
Chuo cha mafunzo ya ufundi (VETA) jijini Dar es Salaam leo.
No comments:
Post a Comment