TAARIFA KWA UMMA JUU YA KUFUTIA
USAJILI VYUO VILIVYOKIUKA TARATIBU ZA USAJILI ZA VETA
UTANGULIZI
Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)
ni chombo cha umma kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 1 ya mwaka 1994 [na
kufanyiwa marekebisho mwaka 2006] kwa ajili ya kuratibu, kudhibiti ubora, kuendeleza, na kugharamia elimu
na mafunzo ya ufundi stadi nchini.
Usajili na Utoaji Ithibati kwa vyuo vya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini ni miongoni mwa wajibu wa VETA katika
kutekeleza jukumu la kuthibiti ubora wa mafunzo ya Ufundi stadi. Vyuo vyote vinavyotoa
mafunzo ya ufundi stadi nchini, vikiwemo vinavyomilikiwa na watu binafsi, taasisi
binafsi, au umma vinapaswa kusajiliwa na kupata ithibati kutoka VETA kabla ya
kuanza kutoa mafunzo.
VIGEZO VINAVYOTUMIKA KUSAJILI
Vigezo vinavyotumika kusajili vyuo vinavyotoa elimu
na mafunzo ya ufundi stadi ni kama vifuatavyo:
- Mitaala: Chuo kinapaswa kutumia mitaala iliyoidhinishwa na Bodi inayosimamia Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi;
- Watumishi (Walimu na wasio walimu): Chuo kinapaswa kuwa na watumishi wa kutosha na wenye viwango vya elimu vinavyowiana na matakwa ya majukumu ya nafasi zao za kazi kama ilivyoanishwa katika miongozo ya kuanzisha vyuo;
- Zana na nyenzo za kufundishia: Chuo kinapaswa kuwa na zana na nyenzo za kutosha kufundishia fani husika kama ilivyoainishwa katika miongozo;
- Miundombinu: Chuo hupaswa kuwa na miundombinu na mazingira yanayofaa na kukidhi vigezo vya utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi kama ilivyoainishwa katika miongozo;
- Vyanzo vya fedha: Chuo hupaswa kuthibitisha kuwa kina vyanzo vya fedha vya kutosha na endelevu kwa ajili ya kutoa elimu na mafunzo yanayotarajiwa; na
- Huduma muhimu: Chuo hupaswa pia kuwa na huduma muhimu zikiwemo maji, umeme, mawasiliano, na usafiri.
VIGEZO VINAVYOTUMIKA KUTOA ITHIBATI
Vigezo vya
kutoa ithibati kwa vyuo ni pamoja na:
- Mafunzo pendekezwa kuwa na mantiki na yenye kuhitajika kwenye soko la ajira;
- Kuwa na miundo mbinu inayowezesha kutoa mafunzo kwa ufasaha na ufanisi;
- Kuwa na zana na nyenzo bora za kufundishia; na
- Kuwa na vifaa vya mawasiliano vinavyosaidia kutoa mafunzo.
- Kuwa na walimu wenye viwango vya elimu vinavyostahili kufundisha mafunzo husika;
- Kuwa na wanafunzi wenye uwezo wa kufuatilia mafunzo kulingana na mitaala husika;
- Kuwa na mfumo mzuri wa usimamizi wa mafunzo;
- Kuwa na mifumo ya ndani ya kudhibiti ubora (internal quality assurance) wa mafunzo;
- Kuwa na utamaduni unaofaa wa uadilifu na uaminifu; na
- Uwezo wa kifedha na kukubalika kwa mafunzo kwenye soko la ajira pamoja na utawala bora wa chuo unaoshirikisha wadau.
MADARAJA YA USAJILI
Usajili hufanyika katika Madaraja manne yaani daraja
A, B, C na D. Vyeti vya usajili
huonyesha daraja la usajili na fani zinazoruhusiwa kutolewa katika chuo
kulingana na uwezo wake. Madaraja hayo na sifa zake ni kama ifuatavyo:
CATEGORY A
|
CATEGORY B
|
CATEGORY C
|
CATEGORY D
|
Chuo chenye uwezo wa kutoa mafunzo kuanzia fani 8 kutoka sekta
tofauti au zaidi na fani 4 kutoka sekta moja. Angalau fani 4 kutoa zaidi ya ngazi ya pili (level II)
|
Chuo
chenye uwezo wa kutoa kuanzia fani 5 toka kwenye sekta tofauti na fani 2 katika
sekta moja. Angalau fani mbili kutolewa mpaka ngazi ya pili (level II)
|
Chuo chenye uwezo wa kutoa kuanzia fani moja kuanzia kufikia ngazi ya pili (Level
II).
|
Chuo chenye uwezo wa kutoa mafunzo kuanzia
moduli moja hadi kufikia ngazi ya kwanza ya mafunzo (Level I).
|
Kwa hivyo, kwa mamlaka iliyonayo na kwa kuzingatia
vigezo vya usajili na ithibati, VETA inautaaarifu umma kuwa vyuo vifuatavyo
vimefutiwa usajili wa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kutokana na kukiuka au
kushindwa kutimiza vigezo na taratibu mbalimbali zinazotakiwa:
Na.
|
Jina la Chuo
|
Namba ya Usajili
|
Sababu za Kufuta Usajili
|
Maagizo ya Hatua za Kuchukua
|
1.
|
Starcom Hotel Academy - IRINGA
|
VET/IRA/PR/2012/C/030
|
Kubadilisha
eneo la kutolea mafunzo kutoka Kilolo kwenda eneo lingine la Iringa mjini
ambalo halijaidhinishwa na VETA
|
Chuo
kiombe upya usajili katika eneo jipya na kwa kuzingatia vigezo.
|
2.
|
Southern College of Tanzania-IRINGA
|
VET/IRA/PR/2013/D/036
|
Kubadilisha
eneo la kutolea mafunzo
|
Chuo
kiombe upya usajili katika eneo jipya na kwa kuzingatia vigezo
|
3.
|
Green
House Technology VTC - DODOMA
|
VET/DOM/PR/2012/D/013
|
Mmiliki
alifunga kituo bila ya kuiariBu ofisi ya VETA Kanda
|
Kurejesha
cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
4.
|
Amani VTC DODOMA
|
VET/DOM/PR/2012/C/005
|
Kubadilisha
chuo kuwa shule ya sekondari
|
Kurejesha
cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
5.
|
Mikukuyumbu VTC - MTWARA
|
VET/MTR/PR/2012/D/007
|
Kubadilisha
chuo kuwa shule ya sekondari
|
Mmiliki
anatakiwa kurejesha cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
6.
|
Mnero VTC- LINDI
|
VET/LND/PR/2012/C/009
|
Upungufu
wa zana na vifaa vya kufundishia pamoja na miundombinu kuwa chini ya kiwango
|
Kurejesha
cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
7.
|
Majority VTC -
MBEYA
|
VET/MBY/PR/2014/D/030
|
Kituo
kilifungwa kutokana na mgogoro wa wamiliki
|
Kurejesha
cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
8.
|
Baraka VTC
DAR ES SALAAM
|
VET/DSM/PR/2012/D/003
|
Kubadilisha
eneo la kutolea mafunzo kutoka Kinondoni Mkwajuni kwenda kwenye eneo lingine.
|
Chuo
kiombe upya usajili katika eneo jipya na kuzingatia vigezo
|
9.
|
Pure Academic of Aesthetics -
DAR ES SALAAM
|
VET/DSM/PR/2012/C/042
|
Kukosa
wanafunzi kutokana na kutoza ada kubwa mno. Chuo kilikuwa kinatoza ada kubwa
na kwa Dola za Kimarekani
|
Kurejesha
cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
10.
|
Lamoon College of Business -
DAR ES SALAAM
|
VET/DSM/PR/2013/C/053
|
Kukosa
Fedha Za Kuendesha Chuo.
Matumizi
mabaya ya fedha yaliyosababisha uhaba mkubwa wa fedha za kuendeshea mafunzo
|
Kurejesha
cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
11.
|
Mpera VTC -
SHINYANGA
|
VET/SHY/PR/2012/C/005
|
Kutozingatia
vigezo vya usajili
|
Kurejesha
cheti cha usajili kwenye ofisi ya VETA ya Kanda
|
WAMILIKI WOTE WA VYUO VYA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI NCHINI
WANAKUMBUSHWA KUZINGATIA VIGEZO, MASHARTI NA TARATIBU ZOTE ZA UTOAJI MAFUNZO NA
UENDESHAJI WA VYUO KAMA ZILIVYOAINISHWA KATIKA MIONGOZI MBALIMBALI INAYOTOLEWA
NA VETA. VETA HAITASITA KUCHUKUA HATUA STAHIKI KWA CHUO CHOCHOTE KITAKACHOENDELEA
KUKIUKA MASHARTI NA TARATIBU ZA KUTOA MAFUNZO YA UFUNDI STADI.
LENGO LA HATUA HIZI NI KUHAKIKISHA KUWA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
STADI YANATOLEWA KOTE NCHINI NI UBORA NA YANAZALISHA WAHITIMU WENYE STADI MAHIRI.
AIDHA WAZAZI NA WADAU WOTE WANAOMBWA KUWASILIANA NA OFISI ZETU ZA KANDA
KATIKA MIKOA ILIYOORODHESHWA KWENYE JEDWARI ILI KUPATA TAARIFA ZA VYUO VYA UFUNDI STADI KABLA YA KUPELEKA VIJANA WAO
KUSOMA.
KANDA YA DSM (D’SALAAM)
P.O.BOX
40274, DSM
Regional Director:
Habib
Bukko
0784
584365
|
KANDA YA MASHARIKI (MOROGORO)
P.O.BOX
1955, Morogoro
Regional Director:
Asanterabi M Kanza
0715 482952
kanzaamani@yahoo.com
vetaeasternzone@veta.go.tz
|
KANDA YA ZIWA – (MWANZA)
P.O.BOX
1983, Mwanza
Regional Director:
Hildegardis
Bitegera
0754
384563
|
KANDA YA KATI (DODOMA)
P.O.BOX 2084, Dodoma
Regional Director:
Ramadhani Mataka
0784 365827
rmataka@veta.go.tz
|
KANDA YA KUSINI MAGHARIBI (MBEYA)
P.O.BOX 2498, Mbeya
Regional Director:
Justine
Rutta
0784
263300
jrutta@veta.go.tz
|
KANDA YA MAGHARIBI (TABORA)
P.O.BOX
1218, Tabora
Regional Director:
Wilhard
Soko
0754
429294
w_soko81@yahoo.com
wsoko@veta.go.tz
|
KANDA NYANDA ZA JUU (IRINGA)
P.O.BOX
818, Iringa
Regional Director:
Suzana
Magani
0784
358782
susanmagani@yahoo.com
|
KANDA YA
KUSINI MAGHARIBI (MTWARA)
P.O.BOX 700, Mtwara
Regional Director:
Kibehele Joseph
0713 232264
|
KANDA YA KASKAZINI (MOSHI
)
P.O.BOX
1738, Moshi
Regional Director:
Angelus
Ngonyani
0773
150540
|
Kwa
taarifa zaidi wasiliana na:
MKURUGENZI MKUU
VETA
Makao Makuu
S.L.P.
2849, Dar es Salaam
Simu:
022 2863407/9
Baruapepe:
info@veta.go.tz
Tovuti:
www.veta.go.tz
|
Tangazo
hili linapatikana kwenye tovuti ya VETA www.veta.go.tz
Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
MKURUGENZI MKUU
VETA Makao Makuu
S.L.P. 2849, Dar es Salaam
Simu: 022 2863407/9
Baruapepe: info@veta.go.tz
Tovuti: www.veta.go.tz
No comments:
Post a Comment