VETA imeweka
utaratibu maalum kwa ajili ya kujiunga ili kupata mafunzo katika vyuo
inavyovimiliki. Utaratibu ni kama unavyoelezwa hapa chini:
VETA hutoa mafunzo ya
muda mrefu na mfupi katika mifumo mbalimbali;
Kwa mafunzo ya muda
mrefu, Vyuo vyote hutangaza nafasi za kujiunga mwezi wa Agosti kila mwaka.
Matangazo hutolewa kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini pamoja na kwenye tovuti ya www.veta.go.tz;
Mwombaji lazima
awe amemaliza elimu ya msingi, sekondari na kuendelea;
Mwombaji huchukua
fomu katika chuo chochote cha VETA kilichopo karibu naye . Fomu hizo zina taarifa ya vyuo
vyote vinavyomilikiwa na VETA, ikiwa ni pamoja na fani zinazofundishwa na
mahali chuo kilipo na kama ni kutwa au bweni;
Mwombaji anaruhusiwa
kufanya mtihani wa kujiunga mkoa aliochukua fomu lakini anaweza kuchagua kusoma
mkoa wowote anaochagua kulingana na mahitaji yake;
Mwombaji anatakiwa
kufanya mtihani wa kujiunga (Aptitude Tests) mwezi Oktoba na wale wanaofanikiwa
kuchaguliwa hupewa taarifa mwezi Decemba ili kuanza masomo Januari mwaka
unaofuata;
Mwombaji
anayefanikiwa hupewa barua ya kujiunga inayofafanua mahitaji yote muhimu.
Mahitaji yanatofautiana toka chuo kimoja hadi kingine na kutegemeana na fani
aliyoomba, na pia kama ni kutwa au bweni;
Kwa utaratibu huu
Mwombaji anaanza kujiunga na daraja la 1(Level 1) ambalo ni daraja la chini.
Waombaji wanaoendelea madaraja ya juu (Level II-III) vigezo ni ufaulu wa daraja
husika unamwezesha kupanda daraja lingine.
Aina ya fani na madaraja zitakazotolewa katika Vyuo vya VETA Mwaka 2019
http://www.veta.go.tz/assets/uploads/c9c79-AINA-YA-FANI-NA-MADARAJA-ZITAKAZOTOLEWA-KATIKA-VYUO-VYA-VETA-MWAKA-2019..pdf
No comments:
Post a Comment