CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Thursday 8 August 2019

Matukio katika picha ni Dkt. Pancras Bujulu Mkurugenzi Mkuu wa VETA akipata maelezo kutoka kwa walimu na wanafunzi alipotembelea banda la VETA katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.



Matukio katika picha ni Dkt. Pancras Bujulu Mkurugenzi Mkuu wa VETA akipata maelezo kutoka kwa walimu na wanafunzi alipotembelea banda la VETA katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.


Katika banda la VETA, wananchi wameweza kupata taarifa mbalimbali kuhusiana na mafunzo ya Ufundi Stadi na kujionea ubunifu wa teknolojia na zana mbalimbali kwa ajili ya kurahisisha shughuli za kilimo na kuongeza uzalishaji.Karibuni sana VETA.
Ujumbe “Kilimo,Mifugo,na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi"


Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu akionyeshwa jinsi gani mashine ya kuchakata na kukata majani kwa ajili ya malisho ya Mifugo  inavyofanya kazi. Mashine hiyo imebuniwa na mwalimu Fredrick Uliki wa chuo cha VETA Kihonda na ina uwezo wa kuchakata tani saba kwa siku




Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu akipata maelezo kutoka kwa mwanafunzi wa fani ya Ushonaji katika Chuo cha VETA Shinyanga Ester Singael(kwanza kushoto) alipotembelea banda la VETA katika maonesho ya Nanenane yaliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu 2019.Katika fani hii vijana wanajifunza kushona nguo za watoto,za akina mama,wanaume,kudarizi,kutengeneza taulo za kike ,Sabuni za aina mbalimbali na teknolojia ya vitambaa.


Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu akipata maelezo kutoka kwa mwalimu Sussack Mbulu wa chuo cha VETA Songea alipotembelea banda la VETA katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu. Mashine hiyo ya kubangua korosho ina uwezo wa kubangua debe tatu kwa siku.


Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu (kushoto) akidadisi jambo juu ya mbegu za kupanda uyoga alipotembelea banda la VETA katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu. Mkurugenzi Mkuu aliongozana na Meneja uhusiano Sitta Peter (Katikati) na Mkurugenzi wa Kanda ya Magharibi Wilhard Soko (Kulia)





No comments:

Post a Comment