Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) CPA. Anthony Kasore,
amewaagiza wasimamizi wa mafunzo ya ufundi stadi kwenye vyuo vya VETA
kuimarisha utoaji mafunzo ya ufundi stadi kuendana na mahitaji ya soko la
ajira.
CPA. Kasore ametoa maagizo hayo wakati wa kikao kilichowakutanisha wajumbe wa Menejimenti ya VETA Makao makuu, Wakurugenzi wa Kanda na wakuu wa vyuo vya VETA kilichofanyika jijini Dodoma leo tarehe 19 Aprili, 2024.
Kasore amesema
Serikali imeiamini VETA kutoa mafunzo ya ufundi stadi hapa nchini, hivyo ni
wajibu wa watendaji wa VETA kutekeleza jukumu hilo kwa weledi.
“nawahimiza kwa dhati kuwa mkatimize jukumu tulilonalo la kutoa mafunzo bora kulingana na mahitaji ya soko la ajira ili tuweze kuzalisha nguvukazi ya vijana bora katika fani,” amesema
CPA Kasore ameeleza
kiu yake ya kuona watumishi wa VETA wanaimarisha ubora wa mafunzo na kasi ya
utoaji mafunzo ili wananchi wote wapate mafunzo hayo kwa ubora na hatimaye kuwa na nguvukazi mahiri kwa
ajili ya kushiriki kwenye shughuli za kiuchumi.
No comments:
Post a Comment