CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Saturday, 7 December 2024

VETA NA KAMPUNI YA FUNDI SMART KUSHIRIKIANA KUTOA MAFUNZO NA KURASIMISHA MAFUNDI WASIO RASMI

 

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) na Kampuni ya Fundi Smart ya jijini Mbeya zimetiliana saini makubaliano ya kushirikiana kutoa mafunzo ya Ufundi na kuwezesha urasimiahaji wa mafundi waliopata ujuzi nje ya mfumo rasmi wa mafunzo.

Makubaliano hayo yamesainiwa jana, tarehe 6 Decemba 2024, katika ukumbi wa VETA Makao Makuu, jijini Dodoma kati ya Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA.Anthony Kasore na Mkurugenzi wa Kampuni ya Fundi Smart, Fredy Herbert Pole.

Wote Kwa pamoja wamekubaliana kuanzisha na kutoa mafunzo Kwa mafundi wasio rasmi (Wanagenzi) na hatimaye kuwarasimisha na kuwatambua kwa viwango vinavyohitajika kwenye stadi husika.





No comments:

Post a Comment