CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Thursday, 20 March 2025

Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda akoshwa na kazi inayofanywa na VETA, ahimiza vijana kuchangamkia fursa

 

Waziri Mkuu mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda ameelezea kufurahishwa na kazi nzuri inayofanywa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) katika utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi yanayowawezesha Watanzania wengi kupata ujuzi wa kujiajiri na kuajiriwa.

Pinda ameyasema hayo jana 20 Machi, 2025 katika maadhimisho ya miaka 30 ya VETA ambapo pia alitembelea mabanda mbalimbali kwenye viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam.

Amebainisha kwamba ufundi stadi ni sehemu ya maisha ya mwanadamu ambapo maendeleo ya Taifa yanategemea ujuzi ambao hakuna mtu anayeweza kukwepa, na amepongeza VETA kwa kazi kubwa waliyoifanya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka hiyo.

“Tumeona mambo mengi mazuri, yanaonyesha dhahiri kwamba tulikokuwa siko tulipo, tumepiga hatua kubwa katika ufundi stadi pamoja na ubunifu mambo ambayo katika maisha ya mwanadamu hawezi kuyakwepa, ni sehemu ya maisha ya mtu, ni sehemu ya maendeleo ya taifa.”

Aidha,ameongeza kwamba,“VETA mnastahili kupewa pongezi kwa kazi kubwa ambayo mmeifanya mpaka sasa, ndani ya mafunzo yanayotolewa utakuta kilimo kipo, ufugaji upo, uvuvi upo. Ukitazama kwenye huduma za jamii afya, elimu yenyewe na vitu vingine mafundi stadi wametoka kwenye vyuo vyetu,”



No comments:

Post a Comment