CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Thursday 30 November 2017

Mfumo wa kusoma kwa njia ya simu VSOMO waanza kutoa matunda.


Mamlaka ya elimu na  Mafunzo ya  ufundi Stadi  (VETA) kwa kushirikiana Kampuni ya simu ya mkononi Airtel kupitia application ya VSOMO wamewatunuku vyeti vijana zaidi ya saba walio hitimu mafunzo hayo kwa njia ya simu.

Akikabidhi vyeti hivyo ,Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Dar es salaam, ndugu Habibu Bukko aliishukuru kampuni ya simu ya Airtel Tanzania  kwa kushirikiana nayo kupitia application ya VSOMO kwani application hiyo imeweza kusaidia wanafunzi kwa kiasi kikubwa hasa wale walio mbali na vyuo vya Ufundi stadi.

Alisema jitiahada za kutoa masomo ya ufundi stadi kupitia application ya VSOMO zinaendana na mikakati iliyojiwekea VETA na serikali kutanua wigo wa kutoa mafunzo ya ufundi stadi.

Alisema Application hii inalenga kufikia vijana walio mbali yaani vijijini ambapo kwao ni ngumu kufikia huduma ya vyuo vya ufundi stadi vya karibu lakini pia sehemu ambapo kuna miundombinu hafifu. 

Pia aliwapongeza vijana hao kwa kutumia vyema simu zao za mkononi kwa ajili ya masomo.  
Akiongea na waandishi Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtell Tanzania Beatrice Singano alisema Airtell wanayo furaha kubwa sana katika kusaidia vijana kupata mafunzo ya Ufundi stadi,

Alisema kwa kupitia programu hii wana uhakika nchi itapata mafundi bora na nguvu kazi ya kutosha kwani wamejifunza kuwa vijana wanaopitia mafunzo haya ni makini na wenye uwezo mkubwa.

Aliendelea kuwahamasisha vijana kudownload application ya VSOMO Kwenye simu zao ili kuweza kupata fursa ya kuweza kupata mafunzo kwa njia rahisi sana.
Naye mwakilishi wa mkuu wa chuo cha VETA Kipawa,Harold Mganga, alisema Mpango huu umevutia vijana zaidi ya 30,000 ambao wameweza kupakua aplication ya VSOMO na kati yao, 9,000 wamejiandikisha kwa masomo
 
Alisema programu ya VSOMO ina lengo la kupanua vikwazo vya VETA kutoa masomo ya ufundi kwa jamii kote nchini.

"Hadi sasa tuna wanafunzi 54 ambao wamekamilisha kozi zao za ufundi na wametunukiwa vyeti," alisema na kuongeza,“hivi karibuni tutakuwa na kundi lingine la wanafunzi wanaomaliza masomona   tayari tuna wanafunzi 25 wanasubiri mafunzo ya vitendo yaliyotarajiwa kuanza hivi karibuni katika vyuo vyetu vya VETA .”

Aliwahimiza vijana kujiandikisha kwa ajili ya mafunzo ya ufundi kupitia simu zao za mkononi na VETA watakuwa katika huduma yao ili kuhakikisha kuwa wanafuatilia mafunzo kwa viwango vya kazi.




No comments:

Post a Comment