Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeandaa mkutano wa wadau kwa lengo la kuwasilisha mpango mkakati wake wa miaka mitano na kupokea maoni yao.
Akifungua warsha hiyo
Dar es Salaam kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi
Stadi Bw Peter Maduki leo tarehe
12/02/2018, Mjumbe wa Bodi hiyo Bw Suleiman Lolila alisema kuwa mpango mkakati
huo unatoa picha halisi ya nini mamlaka hiyo (VETA) inatarajia kufanya ndani ya
miaka mitano.
Alitaja malengo makuu
ya mkakati huo kuwa ni kuboresha utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi ,
kupanua wigo wa utoaji mafunzo ya elimu na ufundi stadi ili kufikia makundi
mengi zaidi na kuimarisha menejimenti ya VETA .
Malengo mengine ni
kupunguza maambukizi wa virusi vya ukimwi na kuboresha huduma saidizi na
kutekeleza mpango wa taifa dhidi ya rushwa.
Aliwataka wadau hao
kutoa mawazo yao ili kuboresha mpango mkakati huo na kwamba Bodi hiyo itapokea
mawazo hayo na kuyajumuisha katika mpango mkakati na kusimamia utekelezaji wake
kwa kuweka mazingira rafiki na kutoa usimamizi wa karibu kuhakikisha malengo
hayo yanafikiwa.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu
wa VETA Dkt. Bwire Ndazi amesema kuwa Mpango mkakakati huo umeandaliwa kwa
kuzingatia hali halisi ya kiuchumi na kijamii ili kuhakikisha ajenda ya
serikali ya kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya viwanda inafikiwa.
“Katika miaka mitano
ijayo (2018/2019 hadi 2022/2023) mamlaka hiyo imejikita katika kuhakikisha
uboreshaji wa utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi ili kuwa na mafundi
stadi mahiri na wa kutosha nchini.
Baadhi ya malengo
ni
Kuongeza
udahili wa wanafunzi katika vyuo vya ufundi stadi kutoka 200,000 hadi 700,000
Udahili
wa watu 400 wenye mahitaji maalum kila mwaka
Udahili
wa vijana 2400 wanaotoka katika mazingira magumu kila mwaka
Kuongeza
udahili wa wanafunzi wa kike kutoka asilimia 35 hadi 45
Utambuzi
na Urasimishaji wa vijana 200,000 waliopata mafunzo kupitia mfumo usio rasmi
No comments:
Post a Comment