Mkuu
wa Chuo cha VETA Mwanza, Charles Kengese (anayenyoosha mkono) akionesha wajumbe
wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) vifaa vilivyonunuliwa kwa ajili
ya karakana ya mafunzo ya ufundi wa umeme wa viwandani wakati wa ziara ya
Kamati hiyo katika chuo cha VETA Mwanza, 26 Machi, 2018. Kushoto kwake ni
Mwenyekiti wa PAC Mh. Naghenjwa Kaboyoka na kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Peter Maduki. Wengine ni Wajumbe wa Kamati
hiyo na maafisa mbalimbali wa serikali na Menejimenti ya VETA.
Mkufunzi wa Chuo cha VETA Shinyanga, Florence Kihundo (kushoto) akiwaelezea wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ubunifu wa utengenezaji wa samani na vifaa mbalimbali kwa kutumia maranda ya mbao, ambao unasaidia utunzaji wa mazingira kwa kupunguza utupaji hovyo wa maranda, wakati Kamati hiyo ilipotembelea katika chuo cha VETA Shinyanga, tarehe 28 Machi, 2018. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa PAC, Mh. Aeshi Hilaly akiangalia kwa makini moja ya vifaa hivyo.
Kaimu
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Bwire
Ndazi (aliyesimama) akitoa maelezo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za
Serikali (PAC) juu ya utekelezaji wa shughuli na miradi mbalimbali ya Mamlaka
wakati wa ziara ya Kamati hiyo katika chuo cha VETA Mwanza, 26 Machi, 2018.
Kulia na kushoto kwake ni maafisa kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na
Teknolojia.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Peter Maduki (kulia) akitoa
maelezo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu
Mafunzo ya Ufundi wa Mitambo Mikubwa yanayoendeshwa katika Chuo cha VETA
Shinyanga wakati Kamati hiyo ilipotembelea karakana ya Ufundi wa Mitambo
Mikubwa katika chuo hicho, tarehe 28 Machi, 2018. Kulia kwake ni Makamu
Mwenyekiti wa PAC Mh. Aeshi Hilaly.
Wajumbe
wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakisikiliza maelezo juu ya
stadi za ukataji na ung’arisha madini na vito, kutoka kwa mwanafunzi wa kozi
hiyo katika chuo cha VETA Shinyanga, wakati wa ziara ya Kamati hiyo kwenye chuo
hicho tarehe 28 Machi, 2018.
Mkuu
wa chuo cha VETA Shinyanga, Afridon Mkhomoi (wa pili kutoka kushoto) akitoa
maelezo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu
Mafunzo ya Ufundi wa Mitambo Mikubwa yanayoendeshwa katika Chuo cha VETA
Shinyanga wakati Kamati hiyo ilipotembelea karakana ya Ufundi wa Mitambo
Mikubwa katika chuo hicho, tarehe 28 Machi, 2018. Kulia mwisho ni Makamu
Mwenyekiti wa PAC Mh. Aeshi Hilaly na kushoto mwisho ni Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu
na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Peter Maduki.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mh. Naghenjwa Kaboyoka (wa pili
kutoka kushoto-mbele) akitoa maneno ya pongezi kwa VETA baada ya kutembelea na kujionea
ujenzi wa karakana ya Mafunzo ya Ufundi wa Umeme wa Viwandani katika chuo cha
VETA Mwanza, tarehe 26 Machi, 2018. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu
na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Peter Maduki na kulia kwake ni Mkuu wa Chuo cha
VETA Mwanza, Charles Kengese.
No comments:
Post a Comment