CONTACT US: VETA Head Office, P.O.Box 802 Dodoma Tanzania, Plot No. 18, Central business Park (CBP). E-mail: info@veta.go.tz / pr@veta.go.tz/ Telephone: +255 26 2963661 Mobile +255 755267489 Fax: +255 22 2863408 / Url: www.veta.go.tz

Friday 17 January 2020

Shiriki MAKISATU 2020



Je wewe ni Mbunifu wa Teknolojia au suala lolote la Kisayansi au Maarifa Asilia?



Karibu ushiriki katika Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU).






Kuhusu MAKISATU: Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) yameanzishwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa lengo la kutambua, kuendeleza na kubiasharisha ubunifu katika sayansi na teknolojia ili kuchangia katika kufikia lengo la Tanzania  kuwa nchi ya uchumi wa kati unaoendeshwa na viwanda.

Kaulimbiu na Kilele cha MAKISATU 2020:  Mashindano hayo yanafanyika mwaka huu yakiwa na Kaulimbiu, “Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwa Uchumi wa Viwanda” na kilele chake kinatarajiwa kufanyika Dodoma mwezi Machi.  

Uratibu wa VETA:  Katika Mashindano hayo, Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) inaratibu mchakato wa mashindano katika ngazi ya Vyuo vya Ufundi Stadi na Sekta Isiyo Rasmi.

Shiriki mashindano: VETA inawakaribisha wabunifu wa Teknolojia na masuala ya Kisayansi au Maarifa Asilia walio kwenye Vyuo vya Ufundi Stadi au Sekta Isiyo Rasmi kushiriki mashindano hayo.  

Mwisho wa kuwasilisha fomu za maombi ni tarehe 31 Januari 2020. Pakua hapaMwongozo na Fomu kwa ajili ya Mashindano hayo.

Kwa maelezo zaidi au ufafanuzi, piga simu au tuma ujumbe kwenda 0736505027 au 0755267489 au Barua pepe pr@veta.go.tz

No comments:

Post a Comment